Doug Burgum
Mandhari
Doug Burgum (Alizaliwa 1 Agosti, 1956) ni mfanyabiashara na mwanasiasa nchini Marekani ambaye amehudumu kama Waziri wa Mambo ya Ndani wa Marekani tangu mwaka 2025 chini ya Rais Donald Trump.[1] Alihudumu kama Gavana wa North Dakota kuanzia mwaka 2016 hadi 2024.[2] Kabla ya siasa, alikuwa mfanyabiashara katika tasnia ya programu za kompyuta; aliuza kampuni yake, ya Great Plains Software, kwa Microsoft mwaka 2001 kwa dola bilioni 1.1.[3] Mnamo Novemba 2024, Rais Trump alimteua kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, na alithibitishwa na Seneti ya Marekani kwa kura 79 dhidi ya 18 mnamo Januari 2025.[4]
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ "President-elect Trump nominates Burgum to serve as Interior Secretary, chair new National Energy Council". North Dakota State Government.
- ↑ "Doug Burgum elected Governor". WDAY. November 10, 2016.
- ↑ "Microsoft Completes Acquisition of Great Plains" (Press release). Microsoft Corp. April 5, 2001.
- ↑ Budryk, Zack (January 30, 2025). "Senate confirms Burgum as Interior secretary". The Hill.