Nenda kwa yaliyomo

Adrien Silva

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Adrien Sébastien Perruchet da Silva (alizaliwa 15 Machi 1989) ni mchezaji wa zamani wa soka la kulipwa aliyekuwa akicheza katika nafasi ya kiungo.

Alianza kazi yake ya soka katika Sporting CP, ambapo alicheza mechi yake ya kwanza na timu ya wakubwa akiwa na umri wa miaka 18.

Katika kipindi cha miaka 10 akiwa Sporting CP, Adrien Silva alicheza mechi 241 na kufunga mabao 39. Pia alisaidia klabu hiyo kushinda kombe la Taça de Portugal mara mbili, mwaka 2008 na 2015.

Kazi ya klabu

[hariri | hariri chanzo]

Miaka ya mwanzo

[hariri | hariri chanzo]

Silva alizaliwa Angoulême, katika eneo la Poitou-Charentes, Ufaransa, akiwa na baba Mreno na mama Mfaransa.

Alianza safari yake ya soka akiwa na umri wa miaka 10 katika klabu ya FC Girondins de Bordeaux. Hata hivyo, baada ya kukaa huko kwa mwaka mmoja, baba yake aliyekuwa akifanya kazi katika sekta ya anga na ndege alirejea Ureno.

Baadaye, familia yao ilihamia na kuishi Arcos de Valdevez, Ureno.[1][2]

  1. https://www.fpf.pt/pt/Jogadores/Adrien-Silva
  2. https://www.national-football-teams.com/player/57770/Adrien_Silva.html
Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Adrien Silva kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.